Posts

Showing posts from February, 2017

Fahamu Kuhusu huduma ya kuhamia mtandao mwingine bila kubadili namba.

Na Abel Msumba, *Huduma  ya  Mobile    Number     portability (MNP) ina maana gani  kwa  mtumiaji* ? Huduma ya kuhamia mtandao mwingine bila kubadili namba ya simu ya kiganjani (MNP), ina maana kuwa mtumiaji anabaki na namba yake ya awali iwapo ataamua kuhamia mtandao mwingine wa simu za kiganjani nchini Tanzania. Kimsingi, ni huduma ambayo inakuwezesha kubakia na namba yako bila kujali unatumia mtandao gani. Hivyo, iwapo utabadilisha mtoa huduma wa simu za kiganjani hutakuwa na haja ya kusumbuka kuwaataarifu watu wako wa karibu – marafiki, familia na wafanyakazi wenzako au washirika wako kwamba umebadilisha namba kwani inabakia ileile. Huduma ya MNP ina faida zipi? Utaendelea kutumia namba yako ya awali unapohama kutoka mtoa huduma mmoja kwenda mwingine na hivyo kufurahia uhuru na utulivu katika matumizi. Utapokea simu na meseji bila kujali ni mtandao upi umehamia na bila kuwa na haja ya kuwataarifu marafiki, familia na ...

Fahamu jinsi ya kuweza ku-root smartphone yako

Image
SOCIAL HALL Home   Afya   Android   Elimu   Mahusiano   Burudani   Video Mpya JINSI YA KUROOT SIMU YAKO (SMARTPHONE) By Abel Msumba Simu zetu za Android zimekua sehemu ya Maisha yetu ya kila siku. Tunazitumia katika Mawasiliano, Kuhifadhi kumbukumbu za muhimu, burudani, biashara, nk. Haya yote hufanywa na Program ambazo huwekwa kwenye mfumo wa simu (Operating System). Programu hizo hubeba maaginzo maalum (Set of instructions) ambazo humwezesha mtumiaji kufanyia mambo mbalimbali kutegemea program hio. Mfano wa program muhimu kwenye simu ni kama vile Opera Mini (humwezesha mtumiaji kufungua kurasa mbalimbali za Intaneti), Calculator, nk. Program hizo huwekwa sio tu kwenye simu, bali hata vifaa vingine kama vile Computer. Mtumiaji wa Simu au Computer ndie anaeamua program ya kuweka kutegemeana na matumizi yake. Katika miongo michache iliopita zimetengenezwa program nyingi mpya na zenye maboresho makubwa na ya kisasa. Ubunifu uliopo katika progr...

Mashabiki Arsenal waamua kuuza tiketi zao

Image
Mashabiki Arsenal waamua kuuza tiketi zao Msumbaabely BLOG /  London, England .Maelfu ya mashabiki wa Arsenal waliokuwa na tiketi za mechi ya marudiano baina ya timu yao na Bayern Munich wameanza kuziuza tiketi hizo baada ya majanga waliyokutana nayo kwenye mechi ya kwanza. Hakukuwa na tiketi yoyote kuhusu mechi hiyo ya Emirates zote zilikuwa zimekwishwa kabla ya mechi yao ya kwanza ya kipigo cha mabao 5-1 huko Allianz Arena, lakini sasa zimeanza kupatikana sokoni. Kikosi hicho cha kocha Arsene Wenger kinahitaji kufanya maajabu kwenye mechi ya marudiano itakayofanyika Machi 7 ili kusonga mbele, lakini hata wale mashabiki wenye roho nguvu wa timu hiyo wanaamini hilo haliwezekani. Kwa kipigo hicho, Arsenal sasa itakwama kuvuka hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya saba mfululizo. Baada ya awali uwanja wa Emirates kuonekana kuwa tiketi zote za mechi zimeuzwa, lakini sasa imefichuka kutakuwa na siti zitakazokuwa wazi kwa sababu mashabiki wa Arsenal wameamua k...

Mambo 8 muhimu ya kuzingatia kutoka kuajiriwa hadi kujiajiri MUUNGWANA BLOG / 13 minutes ago  Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo.  Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri. Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa. Mkakati ni muhimu Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto. Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza ndoto yako, fanya utafiti wa kina kuhusu mipango yako binafsi ya maisha, mtazamo wako kuhusu maisha, mpenzi/mke wako, familia yako, na hali ya jamii kwa ujumla inavyoenda kama vile mabadiliko ya hali ya kisiasa, teknolojia, na uchumi. Tengeneza malengo ya aina ya shughuli unayotaka kuifanya ukiacha kuajiriwa, na pima uwezekano wa shughuli hiyo kufanyika kweli na kama itakulipa. Utambue pia aina ya watu na rasilimali nyingine utakazozihitaji, na jinsi utakavyozipata. Unahitaji fedha Ndio, unahitaji kiasi cha fedha za kutosha kununua vifaa na malighafi za kutengenezea bidhaa yako. Pia unahitaji fedha za kuwalipa wafanyakazi wako, na zaidi sana , unahitaji fedha za kuendesha maisha yako na familia yako , kwa kipindi fulani kabla ya biashara kuanza kukulipa mshahara. Hivyo kabla haujaacha kibarua chako, hakikisha umetengeneza bajeti ya kutosha na una akiba ya kutimiza mahitaji ya bajeti yako. Usingependa uache kazi halafu uanze kuwa omba omba kwa rafiki na jamaa, au uanze kujuta. Network ni muhimu Kumbuka katika kujiajiri kwako, utahitaji wateja, washirika, wafanyakazi na hata washauri mbalimbali ili mambo yako yaende vizuri. Hivyo, wakati ukiwa umeajiriwa ndio wakati wako muafaka wa kutengeneza na kupanua wigo wako wa watu unaowafahamu na waliokaribu nawe. Kumbuka kuendeleza mawasiliano kwani watu hawapendi kuona wewe unataka kuwatumia tuu kisha unawatupa. Endeleza mawasiliano walau hata kwa salamu tuu. Zaidi sana, heshimu watu wote, hata usiowafahamu au wale unaodhani 'sio watu muhimu'. Jenga taswira nzuri kwa jamii kwa lugha fasaha, picha na matukio mengine, usifanye watu wakufikirie vibaya. Usipitwe na wakati: Hakikisha kuwa unafuatilia taarifa za matukio, dili na watu wanaohusiana na aina ya shughuli unayopanga kuifanya wakati utakapojiajiri. Hii itakusaidia kupata uzoefu na kusoma alama za nyakati, na pengine kutambua fursa nyingine zaidi. Endelea kujifunza zaidi kuhusu kazi yako, watu na jamii kwa ujumla kwani kujiajiri kunahitaji uzoefu zaidi, na zaidi sana uwezo wa kupambana na changamoto nyingi ambazo nyingine haujawahi kukutana nazo kabisa, ila taarifa za awali na kujua jinsi mambo yanavyoenda kwa ujumla katika jamii vitakufanya ushinde changamoto. Maana halisi ya biashara Baada ya kuacha kuajiriwa, hautarajii kuwa mtu wa ‘kuganga njaa’ yaani kufanya biashara ili mradi tuu hela iingie, lakini haujui mwelekeo wa biashara yako upoje, na wala hakuna mkakati wa kuikuza na kuimarisha biashara husika. Biashara inahusu kutimiza mahitaji ya watu, kwahiyo ili mradi utakuwa na uwezo mkubwa wa kutimiza mahitaji ya watu, na kuendelea kuhamasisha watu zaidi kuja kwako uweze kutimiza mahitaji yao , basi biashara itakua, na itaendelea kuwa endelevu. Kinyume cha hapo, ushindani utakutoa katika biashara kwani wateja watakambilia kwa wengine. Biashara sio tuu kupata wateja, ni vile kuweza kuendelea kupata wateja na kuendelea kupanua biashara. Inabidi uipende shughuli husika unayoifanya, na uweze kutimiza mahitaji ya wateja kupitia biashara husika. Muda wako mwingi utautumia katika shughuli yako mpya utakayojiajiri hivyo, kama ambavyo kazi uliyonayo pengine ‘inakuboa’, hakikisha ajira yako binafsi ‘haikuboi’. Umuhimu wa wafanyakazi Watendaji wa shughuli husika za biashara yako utakayoianzisha ni muhimu wawe wenye ujuzi na uzoefu wa kutosha wa kufanya shughuli husika, na uweke mikakati ya kuwapatia nyenzo zote muhimu za kufanyia kazi ikiwemo teknolojia na mazingira mazuri ya kazi. Hivyo basi wakati unajiandaa kujiajiri tilia maanani hili katika bajeti yako ya kuajiri. Usingependa wafanyakazi wao wajisikie vibaya kama vile wewe ulivyojisikia vibaya katika ajira yako fulani (pengine ajira yako ya sasa). Muda huu ambao umeajiriwa, ndio muda pia muafaka wa kusaka 'vipaji'- yaani watu ambao utafanya nao kazi utakapojiajiri. Inakuhusu wewe  Mafanikio yako katika kujiajiri yanategemea mambo mengi ila zaidi sana yanakutegemea wewe. Je, nini hasa sababu yako ya kutaka kujiajiri? Ni kweli una bidhaa au huduma haswa ya kupeleka sokoni itakayokufanya iendeshe maisha yako na kuiendeleza biashara husika au ni hasira tuu za jinsi bosi wako anavyokuchulia hapo ofisini kwako, au kwakuwa mshahara ul

Image
Mambo 8 muhimu ya kuzingatia kutoka kuajiriwa hadi kujiajiri, Msumbaabely BLOG / Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo.  Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri. Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa. Mkakati ni muhimu Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto. Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza...

Baadhi ya viongozi wa vijiji wamekamatwa kwa kuhamasisha wananchi kulima Bangi wilayani Muleba.

Image
Baadhi ya viongozi wa vijiji wamekamatwa kwa kuhamasisha wananchi kulima Bangi wilayani Muleba. Msumbaabely BLOG / Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango amewakamata baadhi ya wenyeviti na watendaji wa serikali za vijiji walioshindwa kusimamia miradi ya maendeleo ya jamii kwa lengo la kunusuru janga la njaa na badara yake wamehamasisha wakulima kilimo cha zao haramu la bangi na kutumia mbolea ya kukuzia mazao ya chakula kwenye mimea ya dawa za kulevya kinyume cha sheria za nchi. Watendaji hao wamekamatwa katika operesheni maalumu ya kudhibiti dawa za kulevya iliyohusisha kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Muleba mkoa wa Kagera ambapo watu kumi wamekamatwa wakimiliki mashamba saba ya dawa za kulevya aina ya bangi katika kijiji cha Rwigembe kata ya Ngenge kwa kosa la kutumia mbolea ya serikali iliyotolewa kwa wakulima kusaidia kukuzia mahindi na badala yake mbolea hiyo imetumika kukuzia mimea haramu aina ya bangi kinyume cha sheria za nchi. Baadhi ya wakulima wakab...

Chemical amtolea nje rapa Sterio kuhusu Mapenzi, MSUMBAABELY BLOG/.

Image
Rapa wa kike bongo Chemical ameamua kufunguka ya moyoni na kuweka wazi kuwa sasa hawezi kuwa na mahusiano na rapa Stereo kwani anaona rapa huyo kama hayupo 'serious' Chemical amesema hayo kwenye kipindi cha Planet Bongo ya East Africa Radio na kudai anaona Stereo hamaanishi anachokisema na kuwa hayuko 'serious' kwenye jambo hilo ambalo alikuwa akiliimba sana kupitia vyombo vya habari, kwa sababu hajaona hizo jitihada zake. "Mimi nilisema kama kweli Stereo yupo serious anitafute lakini hajanitafuta, off course amenitafuta kama kunitafuta lakini siyo ile serious, unajua nikimkubali haraka anaweza kunichukulia poa, ila naomba nisema tu Stereo saizi atafute mtu mwingine kama Mungu kapanga tutakutana na kama hajapanga basi tena, pleasee Stereo" alisisitiza Chemical Mbali na hilo, rapa huyo amesema mpaka sasa amefanya kazi na Fid Q pamoja na Mr. Blue na kusema kuwa ni kazi nzuri sana hizo ambazo anasubiri muda wake ufike tu ili aanze kuachia kazi hizo.

VIDEO: Zari atoa siri ya mimba ya mtoto wake wa KIUME

Image
VIDEO: Zari atoa siri ya mimba ya mtoto wake wa kiume ANGALIA VIDEO HAPO CHINI... https://youtu.be/goThtp6N_1s

Kante: Ukitaka ubingwa England msajili huyu jamaa

Image
KUNA wana soka wanaamini Ngolo Kante ndio alistahili kuwa Mwanasoka Bora wa Ligi Kuu England, msimu uliopita. Kutokana na mchango wake wa kuisaidia Leicester City kutwaa ubingwa katika msimu wa 2015/16. Kante anacheza nafasi ya kiungo mkabaji maarufu kwa jina la `mkata umeme’ ukizungumza kwa lugha ya kimpira wa Tanzania. Kiungo huyu ana sifa kuu mbili moja ya kukaba na kunyakua mipira na sifa nyingine ni kutibua pasi za timu pinzani. Ingawa mashabiki wengi walimwaga sifa kwa Jamie Vardy na Riyad Mahrez kuwa ndio walichangia ubingwa wa Leicester City. Vardy alisifiwa kutokana na umahiri wake wa kupiga mabao na kuibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu England na pasi za hatari za Mahrez. Mahrez ndio alipewa tuzo ya kuwa Mwanasoka Bora wa England msimu uliopita. Hata hivyo, chati ya Kante imepanda zaidi msimu huu wakati huu akichezea Chelsea. Si kwa sababu anaing’arisha Chelsea inayoongoza Ligi Kuu England lakini ni kutokana na jinsi Leicester City inavyoyumba. Leicester Ci...

TI.D ATANGAZA KUWA YEYE NI MNYAMA, aingia rasmi kumsaidia Makonda,

Image
Nimekuwa muathirika wa madawa ya kulevya, nimekuja kama kijana aliepotea njia siku za nyuma. Nilikosea sana familia yangu, mama yangu, marafiki na jamii kwa ujumla, naomba mnisamehe. Niko tayari kuunga mkono vita hii, mnyama nimeamua". Hayo ni maneno ya TID wakati alipokaribishwa kuzungumza kwaniaba ya vijana walioathirika na Madawa ya kulevya leo kwenye awamu ya tatu ya mapambano ya dhidi ya biashara ya Dawa za kulevya.

VUGUVUGU LA MADAWA YA KULEVYA

YALIYOJIRI KANISANI KWA MCH. GWAJIMA. Askofu Gwajima: Askari walipekuwa nyumba yangu chumba hadi chumba lakini hawakukuta kitu chochote. Askofu Gwajima: Polisi wale hawawezi kuzungumza sababu wataonekana ni waasi. Mimi namuomba Rais aingilie kati hili suala watu wanateseka. Gwajima: Lengo la Paul Makonda ni kuchafua majina ya watu kwa sababu anazozijua mwenyewe. Askofu Gwajima: Mimi nitawaambia kitu, msilaumu Polisi wala Ofisi ya Rais. Wao hawahusiki na hili ila ni kiumbe mmoja tu ameibuka katikati. Askofu Gwajima: Sijawahi kuvuta sigari, kunywa pombe wala kwenda disko tangu nimezaliwa mimi. Askofu Gwajima: Polisi nao wanateswa kama tunavyoteswa sisi. Wanaambiwa wakapekuwe nyumba yangu japo wanajua hamna kitu ila inabidi waende. Askofu Gwajima: Kamanda Sirro akaniuliza kwa nini nimewekwa kwenye orodha hiyo, nikamwambia ni chuki tu za mtu aliyekaa kwenye kiti chake. Askofu Gwajima: Waliniambia wakanipime kwa Mkemia na walinipima kwa uwazi kabisa. Niliwaambia hata wakikuta pombe ...